Skip to main content

JAMBO AMBALO LINAVURUGA MIPANGO YA WATU WENGI

Watu wengi wamekuwa wakijiuliza sana hili swali; Ndugu yangu wa damu amekataa kunisaidia, sijui nitapata wapi msaada wa kukamilisha huu mpango wangu?  Hili ni swali ambalo wengi hujiuliza pale ambapo mtu waliemtegemea anaposhindwa kuwasaidia na hufanya watu kuzunguka na kuomba ushauri kwa watu wengine. Leo nimeona nikushirikishe hili somo natumaini  litakuwa na mafanikio makubwa  katika kupanga na kutimiza mipango mingi.
                Je, ni mambo gani ambayo unatakiwa ujiandae kabla hujaanza mradi au mpango wako? Katika kufanya jambo lolote  lazima ujiandae na kukamilisha maandalizi hayo ndipo uanze jambo lenyewe;
a)      Fanya utafiti na kamilisha mahitaji yote utakayotumia katika mradi au mpango wako.
b)      Kuandaa namna ya kukabilian na changamoto zitakazojitokeza katikati ya mpango wako
c)       Kuandaa njia mbadala endapo mpango uliopo ukifeli ; (yaani kujiandaa kwaajili ya kukosa au kupata)
Maandalizi yaliyokamilika yanakupa 50% ya kufanikisha mpango wako, na utafanya mambo yako kwa mfumo na mpangilio unaotakiwa. Wengi tunashindwa kufanya maandalizi ipasavyo aidha kwa kuchelewa kufanya, kutokufanya au kufanya nusunusu.

                Katika kupanga na kufanya maandalizi ya mahitaji na mpango mzima  kuna jambo moja ambalo wengi linatufanya tusifanikiwe katika malengo yetu, nalo ni KUTEGEMEA MTU. Sylvia Plath mwandishi wa mashairi wa Marekani aliwahi kusema “If you expect nothing from anybody you are never disappointed” (kama hutegemei kitu kutoka kwa mtu yeyote huwezi kukatishwa tamaa). Kukata tamaa hutokana jambo kufanyika au kutokea au kupata kitu tofauti na ulivyotarajia au ulivopanga.

Watu wengi wanaweka malengo lakini katika kuanda mahitaji ya mradi au mpango wao wanategemea mtu Fulani atawasaidia baadhi ya mahitaji yao ili kuendesha mradi, pale mtu unaemtegemea katika lengo lako akipatwa na tatizo au kushindwa kutekeleza mradi au mpango wako mzima unatetereka na huwezi hata njia mbadala.
                Mda mwingine mtu unaemtegemea hujikweza na kujifanya mfalme au bosi wako, hivyo kukupa masharti au kukunyanyasa kwa namna Fulani na kukufanya uwe mnyonge katika kukamilisha mipango yako. Hali hiyo ikijijenga akilini mwako itapunguza uwezo wako wa kujiamini na kukufanya uwe tegemezi katika mipango yako.

                Wakati mwingine unatakiwa umweleze mpango wako wote bila kuficha jambo ili umshawishi aweze kukusaidia kwa wakati. Hata mipango ile ambayo haikutakiwa watu waijue itakulazimu uwafahamishe wale unaotegemea wakusaidie

Kuweka imani yako au kumtegemea mtu kukamilisha mradi wako itakusababisha ukate tamaa endapo mtu huyo atashindwa kukamilisha hitaji lako. Mtu atakwambia “nilitaka nianzishe biashara lakini nimeenda benki nimekosa mkopo”. Hapo mtu anakata tama ya kuanzisha biashara yake na kuanza kupanga mipango mingine; kwanza amepoteza mda wa maandalizi mengine ambayo tayari ameshayafanya; Pili hajaweza kutimiza lengo lake na kushindwa kutimiza moja ya ndoto zake.

                Fikiria kama huyu mtu akiwa na kila kitu amekiandaa na amejipanga kuukabili mradi au mpango wake? Mtu huyu hawezi kukatishwa tama kwakuwa kila anachokihitaji kukamilisha mpango wake amekiandaa na ana uhakika kipo.
                Unaukumbuka msemo wa Kiswahili usemao HERI KENDA SHIKA KULIKO KUMI NENDA UJE, ridhika na ulichonacho tumia ulichonacho utafanikiwa tu.

Comments

Popular posts from this blog

HATUA 10 ZA KUONGEZA UJASIRI BINAFSI

 Ujasiri ni imani anayokuwa nayo mtu juu ya kufanikiwa kwa lengo lake. Ujasiri huo unaweza ukawa ni wa kutegemea mtu au ujasiri binafsi  ambao unategemea  uwezo wa mhusika katika kutenda jambo flani. Ujasiri huleta furaha katika maisha na  pia huongeza ufanisi wa kazi unazofanya na pia mahusiano mazuri katika familia na jamii kwa ujumla.Ktokuwa na ujasiri hupunguza ufanisi wa kazi na huweza kusababisha msongo wa mawazo. 1.        JITAAMBUE Jichunguze na uweze kufahamu mambo ambayo wewe ni dhaifu na mambo yale ambayo wewe  ni hodari unaweza ukayafanya bila wasiwasi. Pia tambua  vitu gani unavipenda na vitu gani unavyovichukia, pia jitambue  wewe katika jamii unatazamwaje na watu na malengo yako kwa ujumla. Hayo yatakusaidia katika kuepuka mambo yatakayokupa huzuni hivyo kukudhoofisha. 2.        ANZA SIKU YAKO VIZURI Anza siku yako kwa kufuata ratiba ambayo umeipangilia na fuata...

MAMBO MUHIMU KWAKO KIJANA WA LEO.

Habari, najua kama wewe ni kijana kuna wakati unafika unawaza ni njia gani utumie ili ufikie malengo yako. Kila mtu anawaza kufanikiwa kuwa na maisha mazuri kujenga familia bora kutunza wazazi wake vizuri n.k. Mafanikio ya malengo yako hayawezi kupatikana kwa kufanya jambo moja, lazima ufanye mambo mengi mazuri ili mwisho ufike mahali ambapo ulitarajia kufika. Hapa nimekuwekea baadhi ya mambo muhimu yanayoweza kuwa na mchango mkubwa katika safari yako kkuelekea kwenye mafanikio. Upekee. Katika dunia ya sasa yenye maendeleo na mapinduzi katika kila sekta, hakuna kazi au talanta(kipaji) ambacho kina watu wachache kila kazi au talanta ina watu wengi na ushindani mkubwa. Jambo la pekee linaloweza kukusaidia kwa sasa ni upekee, fanya kazi au talanta yako lakini kwa ubora na upekee na ubunifu wa hali ya juu kiasi kwamba utawavutia watu na kushinda ushindani uliopo. Albert Einstein aliwahi kusema “The woman who follows the crowd will usually go no further than the crowd. The woman who wa...

50 REASONS TO READ BOOKS FROM SPEAKING TREE BLOG

Join more than a thousand readers 1. Books help to feel more confident. 2. Books help to travel around the world in the cheapest way. 3. Books develop your personality. 4. Books provide food for thought. 5. Books make you laugh and think. 6. Books draw you towards perfection. 7. Books stimulate creativity. 8. Books bring out writing talent. 9. Books help in communicating. 10. Books clear your vision. 11. Books satisfy your curiosity. 12. Books help you make more choices. 13. Books help you build literary talent. 14. Books do not require any special device to teach. 15. Books increase your attention span. 16. Books are fruitful pastime. 17. Books can be used anytime, anywhere. 18. Books provide entertainment, when others fail. 19. Books make you powerful. 20. Books help you know the 'Whys' and 'Hows' of everything. 21. Books help you to create and spread fun. 22. Books help you travel across time intelligently. 23. Books keep you updated with f...

KUGHAIRISHA KWENYE FAIDA

Kughairisha mambo ndio tabia ambayo inaongoza kusababisha watu wengi kutofikia malengo yao kuliko tabia nyingine yeyote, pia tabia ambayo ni ngumu sana kuiacha kama umekwisha kuwa nayo. Kughairisha mambo hutokana na sababu mbalimbali, sababu kuu ikiwa ni kukosa motisha au msukumo wa ndani yako kufanya jambo, pia sababu nyingine kubwa ni kutopangilia mambo yako binafsi. Watu wengi sana huamini kughairisha ni kitu kibaya kabisa katika maisha, jambo ambalo sio kweli. Uzuri au ubaya wa kughairisha hutegemea jambo unaloghairisha, wakati unaoghairisha, na sababu ya kughairisha. Mara nyingi kughairisha hugharimu pale unapoghairisha kwa kutojisikia kufanya jambo bila sababu yoyote (uvivu wa kufanya). Je, unawezaje kupata faida kwa kughairisha? Mwandishi Brian Tracy katika kitabu chake cha Eat that Frog anasema, Kila mtu hughairisha lakini kinachotofautisha kati ya watu wanaofanikiwa na wasiofanikiwa ni katika mambo wanyoghairisha, wengi wasiofanikiwa hughairisha mambo ambayo huc...

SILAHA YA KUTOLAUMU KUFIKIA MAFANIKIO.

Kila jambo unalolifanya duniani linakuwa na asilimia kadhaa ya kushindwa, ndio maana watu huwa na plani B. Unaweza kufanya jambo kwa uhakika kabisa lakini kitu kidogo sana kikakufanya ushindwe, na hii ndio inafanya watu wafanye vitu kwa umakini na kufikiria sana hasa pale ambapo unania ya kufanikiwa katika mambo yako. Lakini muda mwingine unaweza kuwa umefanya jambo kwa umakini sana bila kukosea lakini ukashindwa kwasababu za mtu mwingine ambae mlikuwa mnashirikiana nae huenda ni kwa uzembe au bahati mbaya lakini mambo ndio yameharibika.  Lawama Katika hali kama hii ndipo watu huanza kutupiana lawama, huyu anamwambia mwingine “Unaona uzembe wako umetutia hasara”, Yule pia anatafuta sababu ya yeye kukosea, anaweza akatupia mpira kwa mwingine au la akalaumu vifaa alivyotumia au miundombinu, ilimradi asionekane mkosaji. Katika kampuni au madaraka Fulani watu hupenda kuwatupia lawama watu wa chini yao kimadaraka, lawama hizi huenda ngazi kwa ngazi mpaka kumfikia mtu wa ...

JOIN US ON TELEGRAM

JOIN US ON TELEGRAM
Join a thousand readers on telegram channel, start a reading habit, get inspired, motivated and learn to win in life.Click on the Image join us