Watu wengi wamekuwa wakijiuliza
sana hili swali; Ndugu yangu wa damu amekataa kunisaidia, sijui nitapata wapi
msaada wa kukamilisha huu mpango wangu?
Hili ni swali ambalo wengi hujiuliza pale ambapo mtu waliemtegemea
anaposhindwa kuwasaidia na hufanya watu kuzunguka na kuomba ushauri kwa watu
wengine. Leo nimeona nikushirikishe hili somo natumaini litakuwa na mafanikio makubwa katika kupanga na kutimiza mipango mingi.
Je,
ni mambo gani ambayo unatakiwa ujiandae kabla hujaanza mradi au mpango wako? Katika
kufanya jambo lolote lazima ujiandae na
kukamilisha maandalizi hayo ndipo uanze jambo lenyewe;
a)
Fanya utafiti na kamilisha mahitaji yote
utakayotumia katika mradi au mpango wako.
b)
Kuandaa namna ya kukabilian na changamoto
zitakazojitokeza katikati ya mpango wako
c)
Kuandaa njia mbadala endapo mpango uliopo
ukifeli ; (yaani kujiandaa kwaajili ya kukosa au kupata)
Maandalizi yaliyokamilika yanakupa 50% ya kufanikisha
mpango wako, na utafanya mambo yako kwa mfumo na mpangilio unaotakiwa. Wengi
tunashindwa kufanya maandalizi ipasavyo aidha kwa kuchelewa kufanya,
kutokufanya au kufanya nusunusu.
Katika
kupanga na kufanya maandalizi ya mahitaji na mpango mzima kuna jambo moja ambalo wengi linatufanya
tusifanikiwe katika malengo yetu, nalo ni KUTEGEMEA MTU. Sylvia Plath
mwandishi wa mashairi wa Marekani aliwahi kusema “If you expect nothing from
anybody you are never disappointed” (kama hutegemei kitu kutoka kwa mtu yeyote
huwezi kukatishwa tamaa). Kukata tamaa hutokana jambo kufanyika au kutokea au
kupata kitu tofauti na ulivyotarajia au ulivopanga.
Watu wengi wanaweka malengo lakini katika kuanda mahitaji
ya mradi au mpango wao wanategemea mtu Fulani atawasaidia baadhi ya mahitaji
yao ili kuendesha mradi, pale mtu unaemtegemea katika lengo lako akipatwa na
tatizo au kushindwa kutekeleza mradi au mpango wako mzima unatetereka na huwezi
hata njia mbadala.
Mda
mwingine mtu unaemtegemea hujikweza na kujifanya mfalme au bosi wako, hivyo
kukupa masharti au kukunyanyasa kwa namna Fulani na kukufanya uwe mnyonge
katika kukamilisha mipango yako. Hali hiyo ikijijenga akilini mwako itapunguza
uwezo wako wa kujiamini na kukufanya uwe tegemezi katika mipango yako.
Wakati
mwingine unatakiwa umweleze mpango wako wote bila kuficha jambo ili umshawishi
aweze kukusaidia kwa wakati. Hata mipango ile ambayo haikutakiwa watu waijue
itakulazimu uwafahamishe wale unaotegemea wakusaidie
Kuweka imani yako au kumtegemea
mtu kukamilisha mradi wako itakusababisha ukate tamaa endapo mtu huyo
atashindwa kukamilisha hitaji lako. Mtu atakwambia “nilitaka nianzishe biashara
lakini nimeenda benki nimekosa mkopo”. Hapo mtu anakata tama ya kuanzisha
biashara yake na kuanza kupanga mipango mingine; kwanza amepoteza mda wa
maandalizi mengine ambayo tayari ameshayafanya; Pili hajaweza kutimiza lengo
lake na kushindwa kutimiza moja ya ndoto zake.
Fikiria
kama huyu mtu akiwa na kila kitu amekiandaa na amejipanga kuukabili mradi au
mpango wake? Mtu huyu hawezi kukatishwa tama kwakuwa kila anachokihitaji
kukamilisha mpango wake amekiandaa na ana uhakika kipo.
Unaukumbuka
msemo wa Kiswahili usemao HERI KENDA SHIKA KULIKO KUMI NENDA UJE, ridhika na
ulichonacho tumia ulichonacho utafanikiwa tu.




Comments
Post a Comment