Skip to main content

HATUA 10 ZA KUONGEZA UJASIRI BINAFSI

 Ujasiri ni imani anayokuwa nayo mtu juu ya kufanikiwa kwa lengo lake. Ujasiri huo unaweza ukawa ni wa kutegemea mtu au ujasiri binafsi  ambao unategemea  uwezo wa mhusika katika kutenda jambo flani. Ujasiri huleta furaha katika maisha na  pia huongeza ufanisi wa kazi unazofanya na pia mahusiano mazuri katika familia na jamii kwa ujumla.Ktokuwa na ujasiri hupunguza ufanisi wa kazi na huweza kusababisha msongo wa mawazo.

1.       JITAAMBUE
Jichunguze na uweze kufahamu mambo ambayo wewe ni dhaifu na mambo yale ambayo wewe  ni hodari unaweza ukayafanya bila wasiwasi. Pia tambua  vitu gani unavipenda na vitu gani unavyovichukia, pia jitambue  wewe katika jamii unatazamwaje na watu na malengo yako kwa ujumla. Hayo yatakusaidia katika kuepuka mambo yatakayokupa huzuni hivyo kukudhoofisha.
2.       ANZA SIKU YAKO VIZURI
Anza siku yako kwa kufuata ratiba ambayo umeipangilia na fuata  mtiririko wa kazi au majukumu  yako kwa wakati na kwa ufanisi. Hiyo itakupunguziaz mawazo na kufanya ujione mshindi katika siku hiyo na kukupa ujasiri waz kufanya majukumu ya kesho.
3.       FANYA MAANDALIZI
Kila jambo unalollipanga katika ratiba hakikisha mazingira ya kulitekeleza jambo yako sawa na mipango ya awali imekaa sawa ili kuitiza vizuri ratiba yako na  hivyo kuona umefanikiwa.
4.       JIKUBALI
Kujikubali ni kupuuza madhaifu uliyonayo na kutumia sehemu ya ubora  wako kama silaha. Kama katika kipengele Fulani uko vizuri sana tumia hicho kipengele kupanga malengo yako na tumia kama  silah katika maisha yako. Mfano, kama mtu una kipaji cha uchekeshaji au kucheza mpira au kipaji cha biashara  tumia hicho kipajji kama  silaha yako ya maisha, utayafunika hata madhaifu  uliyonayo. Amini unaweza katika kila jambo.

5.       PENDA KUJIFUNZA
Pale unapokutana na jambo geni au shughuli ngeni kwako, uliza kwa watu wengine upate kujifunza   au kama ni kazi omba msaada ili upate uzoefu wa kujaz kufanya kazi hiyo. Hii itakupunguzia makosa katika kazi zako na kukuongezea uzoefu katika kazi na shughuli tofauti tofauti.
6.       KUWA NA USO WENYE FURAHA
Uso wenye furaha ni silaha kubwa katika maisha, itakusaidia kukukutanisha na watu  mbalimbali na kukuongezea fursa  za maisha. Pia kuishi na watu vizuri huongezwa na ucheshi na nyuso za furaha.

7.       FANYA MAMBO MEMA
Wakati  ule unapofanya matendo mabaya dhamira na akili yako huwaz haifikiri madhara ya baadae. Hivyo penda kujiepusha naz matendo mabaya mapema ikiwemo marafiki wasioshaurika na makundi mabaya. Hii itakusaidia kuepuka feddheha kwa jamii naz hivyo kuongeza ujasiri na uaminifu kwa jamii inayokuzunguka.
8.       ACHA MAWAZO MABAYA
Mawazo unayofikiria yana mchango mkubwa katika maamuzi yako ya mambo mbalimbali, hivyo kuwa na mawzo mabaya kutakusababishia kutendaz maovu naz  kupoteza mwelekeo wako. Uwaza na kutenda mema roho yako itakuwa na amani na utakuwa na ujasiri.
9.       TOA MSAMAHA
Kuwa  mwepesi wa kusamehe  kutakupunguzia mawzo mengi  yasiyo yaz msingi naz hivyo kufikiria vizuri juu  ya mipango yako na kuitakeleza kwa ufanisi. Amani ya moyo wako pia inapatikana kwa kusamehe, hivyo kusamehe kunamsaada mkubwa katika kujiammini kwako.

10.   SAHAU YALIYOPITA
Mambo yaliyopita yote yasahau hii itakusaidia kupunguza mzigo mkubwa wa kutafakari vipindi vya furaha na huzuni vilivypita na kukufanya uone bado hujafanya mambo mengi ya muhimu hapa  duniani. Mafanikio uliyonayo hutaangalia na pia mabaya na nyakati za huzuni ulizopitia utazisahau na kuongeza hamasa ya kutafta zaidi.
Hatua za kuongeza ujasiri zipo nyingi lakini hizo ni baadhi na unaweza ukazifuata na kufanikiwa katika malengo yako. Ujasiri ni moja yaz silaha kubwa za maisha ya mwanadamu


MKUMBUKE MUUMBA WAKO SIKU ZA UHAI WAKO KABLA MAUTI HAIJAKUKUTA.

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO MUHIMU KWAKO KIJANA WA LEO.

Habari, najua kama wewe ni kijana kuna wakati unafika unawaza ni njia gani utumie ili ufikie malengo yako. Kila mtu anawaza kufanikiwa kuwa na maisha mazuri kujenga familia bora kutunza wazazi wake vizuri n.k. Mafanikio ya malengo yako hayawezi kupatikana kwa kufanya jambo moja, lazima ufanye mambo mengi mazuri ili mwisho ufike mahali ambapo ulitarajia kufika. Hapa nimekuwekea baadhi ya mambo muhimu yanayoweza kuwa na mchango mkubwa katika safari yako kkuelekea kwenye mafanikio. Upekee. Katika dunia ya sasa yenye maendeleo na mapinduzi katika kila sekta, hakuna kazi au talanta(kipaji) ambacho kina watu wachache kila kazi au talanta ina watu wengi na ushindani mkubwa. Jambo la pekee linaloweza kukusaidia kwa sasa ni upekee, fanya kazi au talanta yako lakini kwa ubora na upekee na ubunifu wa hali ya juu kiasi kwamba utawavutia watu na kushinda ushindani uliopo. Albert Einstein aliwahi kusema “The woman who follows the crowd will usually go no further than the crowd. The woman who wa...

50 REASONS TO READ BOOKS FROM SPEAKING TREE BLOG

Join more than a thousand readers 1. Books help to feel more confident. 2. Books help to travel around the world in the cheapest way. 3. Books develop your personality. 4. Books provide food for thought. 5. Books make you laugh and think. 6. Books draw you towards perfection. 7. Books stimulate creativity. 8. Books bring out writing talent. 9. Books help in communicating. 10. Books clear your vision. 11. Books satisfy your curiosity. 12. Books help you make more choices. 13. Books help you build literary talent. 14. Books do not require any special device to teach. 15. Books increase your attention span. 16. Books are fruitful pastime. 17. Books can be used anytime, anywhere. 18. Books provide entertainment, when others fail. 19. Books make you powerful. 20. Books help you know the 'Whys' and 'Hows' of everything. 21. Books help you to create and spread fun. 22. Books help you travel across time intelligently. 23. Books keep you updated with f...

KUGHAIRISHA KWENYE FAIDA

Kughairisha mambo ndio tabia ambayo inaongoza kusababisha watu wengi kutofikia malengo yao kuliko tabia nyingine yeyote, pia tabia ambayo ni ngumu sana kuiacha kama umekwisha kuwa nayo. Kughairisha mambo hutokana na sababu mbalimbali, sababu kuu ikiwa ni kukosa motisha au msukumo wa ndani yako kufanya jambo, pia sababu nyingine kubwa ni kutopangilia mambo yako binafsi. Watu wengi sana huamini kughairisha ni kitu kibaya kabisa katika maisha, jambo ambalo sio kweli. Uzuri au ubaya wa kughairisha hutegemea jambo unaloghairisha, wakati unaoghairisha, na sababu ya kughairisha. Mara nyingi kughairisha hugharimu pale unapoghairisha kwa kutojisikia kufanya jambo bila sababu yoyote (uvivu wa kufanya). Je, unawezaje kupata faida kwa kughairisha? Mwandishi Brian Tracy katika kitabu chake cha Eat that Frog anasema, Kila mtu hughairisha lakini kinachotofautisha kati ya watu wanaofanikiwa na wasiofanikiwa ni katika mambo wanyoghairisha, wengi wasiofanikiwa hughairisha mambo ambayo huc...

SILAHA YA KUTOLAUMU KUFIKIA MAFANIKIO.

Kila jambo unalolifanya duniani linakuwa na asilimia kadhaa ya kushindwa, ndio maana watu huwa na plani B. Unaweza kufanya jambo kwa uhakika kabisa lakini kitu kidogo sana kikakufanya ushindwe, na hii ndio inafanya watu wafanye vitu kwa umakini na kufikiria sana hasa pale ambapo unania ya kufanikiwa katika mambo yako. Lakini muda mwingine unaweza kuwa umefanya jambo kwa umakini sana bila kukosea lakini ukashindwa kwasababu za mtu mwingine ambae mlikuwa mnashirikiana nae huenda ni kwa uzembe au bahati mbaya lakini mambo ndio yameharibika.  Lawama Katika hali kama hii ndipo watu huanza kutupiana lawama, huyu anamwambia mwingine “Unaona uzembe wako umetutia hasara”, Yule pia anatafuta sababu ya yeye kukosea, anaweza akatupia mpira kwa mwingine au la akalaumu vifaa alivyotumia au miundombinu, ilimradi asionekane mkosaji. Katika kampuni au madaraka Fulani watu hupenda kuwatupia lawama watu wa chini yao kimadaraka, lawama hizi huenda ngazi kwa ngazi mpaka kumfikia mtu wa ...

JOIN US ON TELEGRAM

JOIN US ON TELEGRAM
Join a thousand readers on telegram channel, start a reading habit, get inspired, motivated and learn to win in life.Click on the Image join us