Ujasiri ni imani anayokuwa nayo mtu juu ya kufanikiwa kwa lengo lake. Ujasiri huo unaweza ukawa ni wa kutegemea mtu au ujasiri binafsi ambao unategemea uwezo wa mhusika katika kutenda jambo flani. Ujasiri huleta furaha katika maisha na pia huongeza ufanisi wa kazi unazofanya na pia mahusiano mazuri katika familia na jamii kwa ujumla.Ktokuwa na ujasiri hupunguza ufanisi wa kazi na huweza kusababisha msongo wa mawazo. 1. JITAAMBUE Jichunguze na uweze kufahamu mambo ambayo wewe ni dhaifu na mambo yale ambayo wewe ni hodari unaweza ukayafanya bila wasiwasi. Pia tambua vitu gani unavipenda na vitu gani unavyovichukia, pia jitambue wewe katika jamii unatazamwaje na watu na malengo yako kwa ujumla. Hayo yatakusaidia katika kuepuka mambo yatakayokupa huzuni hivyo kukudhoofisha. 2. ANZA SIKU YAKO VIZURI Anza siku yako kwa kufuata ratiba ambayo umeipangilia na fuata...
Comments
Post a Comment