Maisha ya mtafutaji ni ya mateso, shida na raha ambavyo vyote kwa pamoja vina mchango mkubwa wa kukusogeza mbele ili ufikie malengo yako. Hakuna maisha yenye mateso na shida tupu na wala hakuna maisha ya raha pekee, hii ni kwa matajiri, fukara na hata wale wa uchumi wa kati. Tofauti yetu ni aina ya shida na matatizo tunayokutana nayo, maskini ana shida zake anazopambana nazo ambazo tajiri anaona si kitu kwake, vivyo hivyo tajiri nae ana shida zake ambazo maskini huona si kitu. Katika kupita kwenye hizi shida, raha na matatizo mbalimbali mtu usipokuwa makini unaweza ukapoteza uelekeo wako au kuahirisha safari yako kuelekea kwenye mafanikio. Napoleon Hill mwandishi wa kitabu maarufu cha Think and Grow Rich aliwahi kuulizwa kwanini watu wanashindwa kufanikiwa, Hill alijibu akasema kuna mambo matatu yanayofanya mtu asifanikiwe 1; Kushindwa kuendana na watu (jamii inayomzunguka) 2; Kuahirisha na 3; Kuacha kufanya jambo (kughaili). Lakini mimi naomba nikuongezee jambo jingine nal...