Skip to main content

SILAHA YA KUTOLAUMU KUFIKIA MAFANIKIO.

Kila jambo unalolifanya duniani linakuwa na asilimia kadhaa ya kushindwa, ndio maana watu huwa na plani B. Unaweza kufanya jambo kwa uhakika kabisa lakini kitu kidogo sana kikakufanya ushindwe, na hii ndio inafanya watu wafanye vitu kwa umakini na kufikiria sana hasa pale ambapo unania ya kufanikiwa katika mambo yako. Lakini muda mwingine unaweza kuwa umefanya jambo kwa umakini sana bila kukosea lakini ukashindwa kwasababu za mtu mwingine ambae mlikuwa mnashirikiana nae huenda ni kwa uzembe au bahati mbaya lakini mambo ndio yameharibika. 


Lawama

Katika hali kama hii ndipo watu huanza kutupiana lawama, huyu anamwambia mwingine “Unaona uzembe wako umetutia hasara”, Yule pia anatafuta sababu ya yeye kukosea, anaweza akatupia mpira kwa mwingine au la akalaumu vifaa alivyotumia au miundombinu, ilimradi asionekane mkosaji. Katika kampuni au madaraka Fulani watu hupenda kuwatupia lawama watu wa chini yao kimadaraka, lawama hizi huenda ngazi kwa ngazi mpaka kumfikia mtu wa mwisho kimadaraka ambae nae hujaribu kutafuta mbinu ya kuonekana sio mkosaji hivyo kuamua kulaumu mazingira ya kutendea kazi au vifaa ambavyo haviwezi kujitetea.
Kila mmoja humtupia lawama mwenzie

Tabia hii humfanya mtu kuyakwepa majukumu yake na kupelekea kupunguza upeo wake wa kufikiri katika kutatua matatizo, yeye kila tatizo linapokuja akishindwa hutafuta kisingizio. Hii tabia ikijijenga ndani yake hufanya mtu kujiona hana hatia hata pale anapokosea na kupelekea uzembe ambao huzaa uvivu na hatimae umasikini.
Je, suluhisho ni lipi?
ACHANA NA LAWAMA ANZA KUWAJIBIKA KWA KILA KOSA HATA KAMA HUJALISABABISHA WEWE MOJA KWA MOJA.
Jilaumu mwenyewe

Kosa lolote linapotokea katika mazingira yako au jamii yako lazima wewe unahusika iwe kwa moja kwa moja au kwa namna moja ama nyingine unahusika, hivyo CHUKUA WAJIBU KWA KILA TATIZO.
Mfano umeshindwa kukamilisha mpamgo Fulani kiuchumi kwasababu mtu uliemkopesha pesa yako amechelewa au anazungusha kukulipa pesa yako, basi usilaumu kwani wewe pia unawajibika. Kosa lako ni kumwamini mtu ambae si mwaminifu, pia kukopesha pesa ambayo ipo kwenye mipango muhimu, hivyo unatakiwa ukae chini uelewe kosa lako, pata somo katika lile kosa, wakati mwingine hutarudia tena kosa hilo.
Huenda umenunua kifaa cha ofisini kikawa  hakifanyi kazi kama inavyohitajika basi jua ulikosa umakini wakati unanunua hivyo wakati mwingine fanya utafiti kabla ya kufanya manunuzi ya vifaa vyako.
Huenda una rafiki ambae amekusababishia matatizo makubwa katika maisha yako, kaa chini fikiria ulikosea wapi, jifunze, tafakari siku nyingine ufanye nini kuepuka kosa kama hilo.
Mwandishi Brian Tracy katika kitabu chake cha Just Shut up and Do It, anasema lawama huleta mawazo mabaya akilini mwa mtu na humfanya aone kuna watu wengine wanaowajibika na maisha yake, jambo ambalo sio sahihi. Hivyo ili kuondokana na mawazo mabaya pamoja na utegemezi kila unapokutana na changamoto jitamkie “NI WAJIBU WANGU”, hii kauli huamsha akili na kufikiria juu ya suluhisho la hilo jambo.
Maisha ni yako wewe WAJIBIKA KWA kila suala linalokukabili/linalokutatiza, hakikisha kila changamoto inayokukabili unafikiria wewe binafsi unaweza kufanya nini kutumia kile ulichonacho kama mtu mwingine pia atatatua kwa upande wake ni jambo la heri. Kujijengea tabia ya kutatua kila chamgamoto inayokukabili na kuwajibika kwa kila kosa linalotokea, hujenga uwezo wa kufikiri na kutatua matatizo kwa haraka na hivyo kukufanya ufanikiwe katika mipango yako mingi.

NAKUTAKIA UTEKELEZAJI MWEMA.

Usichoke Kujifunza.

Comments

Popular posts from this blog

HATUA 10 ZA KUONGEZA UJASIRI BINAFSI

 Ujasiri ni imani anayokuwa nayo mtu juu ya kufanikiwa kwa lengo lake. Ujasiri huo unaweza ukawa ni wa kutegemea mtu au ujasiri binafsi  ambao unategemea  uwezo wa mhusika katika kutenda jambo flani. Ujasiri huleta furaha katika maisha na  pia huongeza ufanisi wa kazi unazofanya na pia mahusiano mazuri katika familia na jamii kwa ujumla.Ktokuwa na ujasiri hupunguza ufanisi wa kazi na huweza kusababisha msongo wa mawazo. 1.        JITAAMBUE Jichunguze na uweze kufahamu mambo ambayo wewe ni dhaifu na mambo yale ambayo wewe  ni hodari unaweza ukayafanya bila wasiwasi. Pia tambua  vitu gani unavipenda na vitu gani unavyovichukia, pia jitambue  wewe katika jamii unatazamwaje na watu na malengo yako kwa ujumla. Hayo yatakusaidia katika kuepuka mambo yatakayokupa huzuni hivyo kukudhoofisha. 2.        ANZA SIKU YAKO VIZURI Anza siku yako kwa kufuata ratiba ambayo umeipangilia na fuata...

MAMBO MUHIMU KWAKO KIJANA WA LEO.

Habari, najua kama wewe ni kijana kuna wakati unafika unawaza ni njia gani utumie ili ufikie malengo yako. Kila mtu anawaza kufanikiwa kuwa na maisha mazuri kujenga familia bora kutunza wazazi wake vizuri n.k. Mafanikio ya malengo yako hayawezi kupatikana kwa kufanya jambo moja, lazima ufanye mambo mengi mazuri ili mwisho ufike mahali ambapo ulitarajia kufika. Hapa nimekuwekea baadhi ya mambo muhimu yanayoweza kuwa na mchango mkubwa katika safari yako kkuelekea kwenye mafanikio. Upekee. Katika dunia ya sasa yenye maendeleo na mapinduzi katika kila sekta, hakuna kazi au talanta(kipaji) ambacho kina watu wachache kila kazi au talanta ina watu wengi na ushindani mkubwa. Jambo la pekee linaloweza kukusaidia kwa sasa ni upekee, fanya kazi au talanta yako lakini kwa ubora na upekee na ubunifu wa hali ya juu kiasi kwamba utawavutia watu na kushinda ushindani uliopo. Albert Einstein aliwahi kusema “The woman who follows the crowd will usually go no further than the crowd. The woman who wa...

50 REASONS TO READ BOOKS FROM SPEAKING TREE BLOG

Join more than a thousand readers 1. Books help to feel more confident. 2. Books help to travel around the world in the cheapest way. 3. Books develop your personality. 4. Books provide food for thought. 5. Books make you laugh and think. 6. Books draw you towards perfection. 7. Books stimulate creativity. 8. Books bring out writing talent. 9. Books help in communicating. 10. Books clear your vision. 11. Books satisfy your curiosity. 12. Books help you make more choices. 13. Books help you build literary talent. 14. Books do not require any special device to teach. 15. Books increase your attention span. 16. Books are fruitful pastime. 17. Books can be used anytime, anywhere. 18. Books provide entertainment, when others fail. 19. Books make you powerful. 20. Books help you know the 'Whys' and 'Hows' of everything. 21. Books help you to create and spread fun. 22. Books help you travel across time intelligently. 23. Books keep you updated with f...

KUGHAIRISHA KWENYE FAIDA

Kughairisha mambo ndio tabia ambayo inaongoza kusababisha watu wengi kutofikia malengo yao kuliko tabia nyingine yeyote, pia tabia ambayo ni ngumu sana kuiacha kama umekwisha kuwa nayo. Kughairisha mambo hutokana na sababu mbalimbali, sababu kuu ikiwa ni kukosa motisha au msukumo wa ndani yako kufanya jambo, pia sababu nyingine kubwa ni kutopangilia mambo yako binafsi. Watu wengi sana huamini kughairisha ni kitu kibaya kabisa katika maisha, jambo ambalo sio kweli. Uzuri au ubaya wa kughairisha hutegemea jambo unaloghairisha, wakati unaoghairisha, na sababu ya kughairisha. Mara nyingi kughairisha hugharimu pale unapoghairisha kwa kutojisikia kufanya jambo bila sababu yoyote (uvivu wa kufanya). Je, unawezaje kupata faida kwa kughairisha? Mwandishi Brian Tracy katika kitabu chake cha Eat that Frog anasema, Kila mtu hughairisha lakini kinachotofautisha kati ya watu wanaofanikiwa na wasiofanikiwa ni katika mambo wanyoghairisha, wengi wasiofanikiwa hughairisha mambo ambayo huc...

JOIN US ON TELEGRAM

JOIN US ON TELEGRAM
Join a thousand readers on telegram channel, start a reading habit, get inspired, motivated and learn to win in life.Click on the Image join us