Skip to main content

Posts

Showing posts from June, 2016

HATUA ZA KUTOA MSAMAHA

Kusamehe ni jambo ambao sio rahisi kulifanya hasa pale unapofikiria kuwa aliekukosea amefanya makusudi ili kukuumiza. Lakini ili usiendelee kuumia unatakiwa kufanya jambo moja nalo ni kusamehe. Wengi husamehe lakini baadae huendeleza chuki na hasira juu ya mhusika jambo ambalo sio sahihi, unapotoa msamaha unatakiwa kuondoa hasira na chuki juu ya Yule alie kukosea. Kwakuwa kusamehe ni   jambo ambalo huhitaji moyo wenyewe uondoe fikra mbaya zote ulizokuwa nazo juu ya Yule mtu, unaweza kufanya yafuatayo ili uweze kusamehe. 1.      ONDOKA ENEO LA TUKIO Kama mtu amekukosea ondoka hiyo sehemu, wakati huo unakuwa na hasira hivyo ukibaki eneo la tukio unaweza   kufanya   maamuzi ya ajabu. Hivyo kaa mbali ili kupunguza hasira, pata utulivu kwa kufanya jambo unalolipenda mfano:- kusikiliza muziki, kutembea ufukweni au kutulia sehemu unayoona wewe utaweza kutulia.   2.      FIKIRIA TUKIO LILIVOKUWA KWA UPANDE WAKO Tuliza akili ...

YAFAHAMU HAYA KUHUSU KUSAMEHE

Kusamehe ni kitendo cha kuondoa hasira, maumivu na hisia unazokuwa nazo baada ya kukosewa. Kila binadamu anapokosewa huona ameonewa na sio haki kile alichofanyiwa hivyo huwa na hasira na hisia za maumivu. Kila lile jambo au tendo linapojirudia akilini mwake hupata maumivu moyoni, hukosa furaha amani na hata kupata msongo wa mawazo. Njia ya kuondokana na maumivu hasira na mawazo yote ni kusamehe. Hapa ndipo wengi huona ni jambo gumu, pale ambapo mtu amekukosea sana halafu wewe uje umsamehe kirahisi tu. Wengi huona sio haki na kuchukua uamuzi wa kulipiza kisasi. Yafahamu haya kuhusu kusamehe:-   1.       KUSAMEHE NI KUJIPENDA MWENYEWE Unapotoa msamaha unaondoa hasira maumivu na mawazo yote uliyonayo juu ya Yule mtu alie kukosea, hivyo kuweka huru moyo wako na akili yako.   Kubaki na hasira, maumivu na hasira ni hasara kwako kwani huhatarisha afya yako. 2.       USISUBIRI MPAKA UOMBWE MSAMAHA Watu wengi kusamehe mpaka...

HATUA 10 ZA KUONGEZA UJASIRI BINAFSI

 Ujasiri ni imani anayokuwa nayo mtu juu ya kufanikiwa kwa lengo lake. Ujasiri huo unaweza ukawa ni wa kutegemea mtu au ujasiri binafsi  ambao unategemea  uwezo wa mhusika katika kutenda jambo flani. Ujasiri huleta furaha katika maisha na  pia huongeza ufanisi wa kazi unazofanya na pia mahusiano mazuri katika familia na jamii kwa ujumla.Ktokuwa na ujasiri hupunguza ufanisi wa kazi na huweza kusababisha msongo wa mawazo. 1.        JITAAMBUE Jichunguze na uweze kufahamu mambo ambayo wewe ni dhaifu na mambo yale ambayo wewe  ni hodari unaweza ukayafanya bila wasiwasi. Pia tambua  vitu gani unavipenda na vitu gani unavyovichukia, pia jitambue  wewe katika jamii unatazamwaje na watu na malengo yako kwa ujumla. Hayo yatakusaidia katika kuepuka mambo yatakayokupa huzuni hivyo kukudhoofisha. 2.        ANZA SIKU YAKO VIZURI Anza siku yako kwa kufuata ratiba ambayo umeipangilia na fuata...

AHSANTE BABA NA MAMA

Siku zote tumezoea kusikia majina ya watangazaji redioni na hata kwenye televisheni kwa kuwa wao ndio wana uhusiano wa moja kwa moja na hadhira (wasikilizaji na watazamaji), lakini nani amezoea kusikia majina ya mafundi mitambo au wachukua picha (camera man)? Ni nadra sana kusikia majina ya hawa watu, japo nao wana mchango mkubwa katika kufikisha matangazo yale kwa hadhira. Hivyo ndivyo ilivo hata kwa wazazi wetu, mama ni mzazi ambae mda wote yupo karibu na mtoto na huduma nyingi mtoto anazipata toka kwa mama na baba ni mtu wa mihangaiko huonana na watoto mara chache zaidi kuliko mama, lakini hii haina maana kwamba baba hahusiki kwenye malezi ya huyu mtoto la hasha ila analea kupitia mgongo wa mama. Mtoto anajua kila kitu analeta mama kwakuwa haoni huduma za baba, lakini tambua kwamba huo uji anaokupikia mama ni baba alietafuta unga. Ni kweli mda mwingine mzazi mmoja anakuwa mzembe katika majukumu, hilo lipo kwa pande zote mama na hata baba anaweza akatelekeza watoto wake ...

JOIN US ON TELEGRAM

JOIN US ON TELEGRAM
Join a thousand readers on telegram channel, start a reading habit, get inspired, motivated and learn to win in life.Click on the Image join us