Kuna mambo mengi madogo madogo lakini ya MUHIMU katika kutimiza mambo yako ya kila siku, mambo hayo wengi hawayatilii maanani aidha kwakuwa hawajui umuhimu wake au wanayapuuza. Mimi huwa namfananisha mtu mwenye ndoto au malengo kama DEREVA na ndoto yake au malengo yake ni kama MZIGO ambao inabidi aufikishe sehemu husika. Kila Dereva huwa anatamani awahi kufika anakoelekea ili apate mshahara wake, shauku ya zawadi au mshahara wake ndiyo inayomfanya afanye juhudi kwa nguvu na ujuzi alionao ili afikishe mzigo kwa wakati mwafaka. Lakini njiani anazingatia alama mbalimbali za barabarani zinazomuongoza afike salama. Hata katika maisha yetu kuna mambo mbalimbali tunayotakiwa tuyatumie ili kufika salama na pia kwa wakati, mambo haya yanatupa tahadhari juu ya yaliyo mbele yetu. Je, katika mipango yako ya maisha iwe biashara, kilimo, Elimu, Sanaa yako huwa unahusisha na taarifa za utabiri wa mamlaka za sekta husika. Wewe ni mkulima je unafuatilia matangazo na tahadhari zinazotolewa n...