Kughairisha
mambo ndio tabia ambayo inaongoza kusababisha watu wengi kutofikia malengo yao
kuliko tabia nyingine yeyote, pia tabia ambayo ni ngumu sana kuiacha kama
umekwisha kuwa nayo. Kughairisha mambo hutokana na sababu mbalimbali, sababu
kuu ikiwa ni kukosa motisha au msukumo wa ndani yako kufanya jambo, pia sababu
nyingine kubwa ni kutopangilia mambo yako binafsi.
Watu
wengi sana huamini kughairisha ni kitu kibaya kabisa katika maisha, jambo
ambalo sio kweli. Uzuri au ubaya wa kughairisha hutegemea jambo unaloghairisha,
wakati unaoghairisha, na sababu ya kughairisha. Mara nyingi kughairisha
hugharimu pale unapoghairisha kwa kutojisikia kufanya jambo bila sababu
yoyote (uvivu wa kufanya).
Je,
unawezaje kupata faida kwa kughairisha?
Mwandishi
Brian Tracy katika kitabu chake cha Eat that Frog anasema, Kila mtu hughairisha
lakini kinachotofautisha kati ya watu wanaofanikiwa na wasiofanikiwa ni katika
mambo wanyoghairisha, wengi wasiofanikiwa hughairisha mambo ambayo huchangia
80% ya maisha yao, wakati wale wanaofanikiwa hughairisha mambo ambayo huchangia
20% katika maisha yao.
Mara
nyingi mambo amabayo ni ya muhimu sana huwa na vikwazo na ugumu katika
kuyafanya hivyo usipokuwa na msukumo kutoka ndani ya nafsi yako ni rahisi kughaili
na kukimbilia katika mambo ambayo yana umhimu kidogo katika maisha yako na mara
nyingi mambo haya huwa rahisi na yasiyo na vikwazo katika kuyafanya.
Ili uweze kutumia
kughairisha kwenye faida katika maisha yako ya kila siku kwanza unahitaji mambo
yafuatayo:-
- UTAMBUA MAMBO MUHIMU KATIKA MAISHA YAKO.
Jitambue kwanza wewe ni nani? Lengo lako hapa
duniani ni lipi? Na unaelekea wapi?
Kisha orodhesha mambo/shughuli za muhimu ambazo
zitakufikisha zitakupeleka huko unakotaka kufika. Mambo ambayo yanachangia
asilimia 80 ya maisha unayotaka kuyaishi hayo ndio mambo muhimu, haya ni mambo
ambayo ni ya kuyapa vipaumbele ukilinganisha na mambo mengine.
- RATIBA YA SHUGHULI ZAKO ZOTE.
Kuwa na ratiba ya shughuli zote unazohitaji
kuzifanya katika siku, wiki na mwezi. Ukishaziorodhesha shughuli zote,
unatakiwa kuzipanga shughuli hizo kwa mtiririko kulingana na umuhimu, uhitaji
na uharaka wa shughuli hizo. Shughuli za muhimu na ambazo zinahitajika
kukamilisha haraka zikae mwanzoni na zile ambazo hata ukikosa muda unaweza
kufanya siku inayofuata zikae mwishoni mwa orodha.
- KUWA NA UTARATIBU MAALUMU WA KUPOKEA MAMBO.
Je, ukipewa taarifa au jukumu la kufanya ambalo
hukuliweka kwenye ratiba unafanyaje? Au rafiki yako akikupa taariafa ya
kukutembelea ghafla unafanyaje? Lazima uwe na utaratibu maalumu ambao hata watu
wengine yaani ndugu, jamaa na rafiki wanatambua kuwa nikitaka kumfuata Fulani natakiwa
kufanya hivi kabla. Kwa kifupi usiwe mtu wa ndio kila wakati. Kwa upande wa
dharura ambazo ni za muhimu sana lazima uwe na uratibu wake pia. Ni kawaida
katika maisha kutokea dharura na mara nyingi dharura hutukuta tukiwa
hatujajiandaa, lakini pia ni muhimu kupima dharura hizo hivyo unatakiwa kuwa na
utaratibu maalumu wa kupokea.
Hivyo katika kughairisha kwenye faida, ukiwa na
mambo mawili au zaidi ambayo yanahitajika kufanyika kwa wakati mmoja, kitu cha
kwanza unaangalia je lipi ni jambo ambalo ni muhimu zaidi kwako?, cha pili ni
je jambo lipi liko kwenye ratiba yako? (Kati ya lile lililopo kwenye ratiba na
lile lililokujia kama dharura lipi la muhimu zaidi kwako katika maisha), cha
tatu je, utaratibu wako wa kupokea jambo kama hilo ni upi?
Unaweza kughairisha kwenda matembezini kwasababu
rafiki yako amekuja na anataka msome pamoja kitabu kipya alichokuletea, Lakini
pia mwingine anaweza kutokughairisha kwenda matembezini kwasababu anaenda
kufanya utafiti wa biashara mpya katika matembezi yake, hivyo akamkatalia
rafiki yake kwakuwa kusoma kitabu hakukuwa kwenye ratiba yake.
Maisha ni jinsi wewe mwenyewe unavyoyapangilia na
kuyaishi.
Kila la kheri katika shughuli zako za kila siku,
USICHOKE KUJIFUNZA.

Comments
Post a Comment