Watu wengi wamekuwa wakijiuliza sana hili swali; Ndugu yangu wa damu amekataa kunisaidia, sijui nitapata wapi msaada wa kukamilisha huu mpango wangu? Hili ni swali ambalo wengi hujiuliza pale ambapo mtu waliemtegemea anaposhindwa kuwasaidia na hufanya watu kuzunguka na kuomba ushauri kwa watu wengine. Leo nimeona nikushirikishe hili somo natumaini litakuwa na mafanikio makubwa katika kupanga na kutimiza mipango mingi. Je, ni mambo gani ambayo unatakiwa ujiandae kabla hujaanza mradi au mpango wako? Katika kufanya jambo lolote lazima ujiandae na kukamilisha maandalizi hayo ndipo uanze jambo lenyewe; a) Fanya utafiti na kamilisha mahitaji yote utakayotumia katika mradi au mpango wako. b) Kuandaa namna ya kukabilian na changamoto zitakazojitokeza katikati ya mpango wako c) ...