Skip to main content

UKIWA MTU WA KIPEKEE/WA TOFAUTI.

Umewahi kujiuliza ni kitu gani cha pekee ambacho kinakutambulisha katika jamii unayoishi?. Kuna watu katika jamii yoyote wanakuwa maarufu kwa tabia au matendo ya tofauti, wakati mwingine wanapewa mjina ya utani kutokana na matendo au tabia hizo. Ukiwachunguza kwa makini hata katika utendaji wao wa majukumu mbalimbali huwa ni wa tofauti sana na watu wengine, wao mara nyingi huwa na upekee katika mambo yao. Je, wewe utofauti wako ni upi katika matendo, mawazo, na malengo yako?

Katika nyakati hizi ambazo utandawazi na tekinolojia vimetawala sana, habari na taarifa zinaenea kwa haraka sana na kufanya mambo mengi kuwa ya wazi zaidi, ushabiki wa watu maarufu umeongezeka na kuenea sana. Katika mambo ambayo yameenda sambamba na kuenea na kukua kwa utandawazi ni KUIGA/KUFUATISHA. Watu wengi wamekuwa wakifanya mambo kwa kuiga au kufuata watu maarufu au watu wengine wanaowaamini, muda mwingine mpaka watu wanashindwa kuwatofautisha kuanzia mavazi mpaka matendo mtu anaiga.

Kuna usemi niliuandika katika somo la MAMBO MUHIMU KWAKO KIJANA WA LEO unaosema Albert Einstein aliwahi kusema “The woman who follows the crowd will usually go no further than the crowd. The woman who walks alone is likely to find herself in place no one has ever been before” (mwanamke anaefuata kundi hawezi kwenda mbali zaidi ya lile kundi. Mwanamke anaetembea pekeake anaweza kufika mahali ambapo hakuna mtu aliewahi kufika pale kabla). Angali watu waliofanikiwa wengi walifanya mambo ya tofauti nay a kipekee; Mfano tajiri wa kwanza duniani kwa sasa aliamua kuacha chuo cha Harvard (moja kati ya vyuo bora duniani) mwaka 1975 akiwa na miaka 20 na kuanza kujihusisha na mambo yake mwenyewe. Hivyo ili ufanikiwe lazima ufanye kitu ambacho ni tofauti na wengine na utafika mahali ambapo wengine hawajafika na hayo ndio mafanikio.

Katika jamii yoyote kuna mtu anaefahamika sana kutokana na umbo lake (Mnene, Mfupi, mweupe kuliko wote n.k) au kutokana na matendo yake, tabia yake ya kipekee na kadhalika. Ukiwa kipekee lazima watu watakufahamu popote uendapo, kile kitu cha kipekee kitakuwa ni alama ya utambulisho wako kwa wengine. Kufahamika ni moja ya nyenzo au silaha muhimu kwa mtu unaeanza kupigana kuelekea mafanikio yako. Kumbuka lazima uwe mtu wa pekee ili uweze kufahamika na kujenga heshima katika jamii yako.

Mtu yeyote katika dunia anakuwa na malengo na ndoto ambazo anapenda zitimie, ndoto ulizonazo wewe hazifanani na ndoto za mtu mwingine hata kama mtafanana malengo yenu. Kila mmoja anafikiria na anafanya juhudi ili kuifikia ndoto yake ya maisha. Ndugu, ukiishi kwa kuiga anachofanya mtu fulani huwezi kufikia ndoto yako ya maisha, utaishia kupotea kwakuwa huyo unaemfuata matendo, tabia au ratiba yake hujui ndoto yake wala fikra zake. Unahitaji kuishi maisha yako halisi, ufuate ndoto yako na hapo utaona namna unavofanikiwa na kufikia ndoto zako. Ili utimize ndoto na malengo yako lazima uiishi nafsi yako kuanzia matendo, tabia, na ratiba yako. Lazima uthamini mawazo na fikra zako mwenyewe, lazima uwe na mtindo wako.

Vijana wengi kwa sasa wamerundikana katika fani za usanii na utumbuizaji, hata vijana wengine wenye elimu ya juu waliokosa ajira wamekimbilia huko. Baadhi ya vijana wamebaki mitaani wakisubiri kazi huku wakijiuliza VIPAJI VYAO NI VIPI??. Haya yote yanatokana na kuishi maisha ya kuiga au kufuata mtu Fulani, huenda kwa sasa humfuati wala kuiga mtu yeyote lakini kuna mtu ulikuwa unamfuata na sasa unatambua umeshapoteza njia kuelekea kwenye ndoto na malengo yako. Huwezi kutambua kipaji chako kama unaishi kwa kumfuata maisha ya mtu mwingine, lazima utapotea na ukija kutambua umeshachelewa na umri  umeenda. Ishi maisha yako ishi nafsi yako ili uweze kutambua na kumudu kipaji chako.

Ben alikuwa ni mwanafunzi katika shule moja ya sekondari ambae alikuwa na malengo na ndoto zake za kutimiza katika maisha yake. Shule hiyo ilikuwa ni ya bweni akawa akiamka asubuhi saa kumi alfajiri anaenda darasani na kusoma hadi saa kumi na mbili anarudi bwenini na kujiandaa kwaajili ya kuingia darasani kama wanafunzi wengine. Hiyo ikawa ndio ratiba yake ya kila siku, lakini kila siku akiingia darasani saa kumi alfajiri alikuwa anamwona kijana mmoja anajisomea, akajua huyo mwanafunzi anajisomea masomo ya shule hivyo hakumfuatilia kwakuwa yeye alikuwa akijisomea vitabu vya masomo ya maisha hasahasa vitabu vya ujasiriamali, ufugaji na kilimo cha kisasa. 
Siku moja Ben aliamka alfajiri na mapema na kwenda darasani kama kawaida yake alipofika hakumwona Yule mwanafunzi aliezoea kumwona anawahi kila siku, lakini Ben hakujali alifungua kitabu chake na kuanza kusoma. Nusu saa baadae Yule mwanafunzi aliingia na kumkuta Ben alishawahi kufika, alipita alipo Ben na kumpa salamu na kwenda kukaa kwenye kona ya darasa kama mazoea yake ya kila siku. Ben aligeuka kumwangalia vizuri Yule mwanafunzi sio kwamba alikuwa hamfahamu, la hasha kuna kitabu alimwona amekibeba na kilikuwa ni moja ya vitabu anavyovitafuta sana. Aliamua kusimama na kumfuata Yule mwanafunzi na kuanza kuzungumza nae. Kila mmoja akatambua malengo ya mwenzake kuwa nje ya masomo muda wa alfajiri wote huwa wanajisomea masomo ya ziada, ukawa ni mwanzo wa wao kuwa na ukaribu kuazimana vitabu na majadiliano ya maada mbali mbali. Kwa sasa Ben anamiliki kampuni ya kusindika mzao mbalimbali na rafiki yake ni anamiliki kampuni ya usafirishaji aliyorithi kwa baba’ke.
Umejifunza nini katika hadithi hii fupi?


Ukiishi maisha yako halisi na kufanya juhudi za kufikia malengo yako, katika harakati zako utakutana na watu wanaoendana na malengo yako, utakutana na marafiki ambao wanafanana ratiba na malengo, hiyo itakusaidia kukupa moyo na kukutia hamasa ya kuzidi kusonga mbele.

MAWAZO, MALENGO NA JUHUDI PEKEE HAVITOSHI KUTIMIZA NDOTO ZAKO,
TANGULIZA SALA KWA MUUMBA WAKO.

Comments

Popular posts from this blog

HATUA 10 ZA KUONGEZA UJASIRI BINAFSI

 Ujasiri ni imani anayokuwa nayo mtu juu ya kufanikiwa kwa lengo lake. Ujasiri huo unaweza ukawa ni wa kutegemea mtu au ujasiri binafsi  ambao unategemea  uwezo wa mhusika katika kutenda jambo flani. Ujasiri huleta furaha katika maisha na  pia huongeza ufanisi wa kazi unazofanya na pia mahusiano mazuri katika familia na jamii kwa ujumla.Ktokuwa na ujasiri hupunguza ufanisi wa kazi na huweza kusababisha msongo wa mawazo. 1.        JITAAMBUE Jichunguze na uweze kufahamu mambo ambayo wewe ni dhaifu na mambo yale ambayo wewe  ni hodari unaweza ukayafanya bila wasiwasi. Pia tambua  vitu gani unavipenda na vitu gani unavyovichukia, pia jitambue  wewe katika jamii unatazamwaje na watu na malengo yako kwa ujumla. Hayo yatakusaidia katika kuepuka mambo yatakayokupa huzuni hivyo kukudhoofisha. 2.        ANZA SIKU YAKO VIZURI Anza siku yako kwa kufuata ratiba ambayo umeipangilia na fuata...

MAMBO MUHIMU KWAKO KIJANA WA LEO.

Habari, najua kama wewe ni kijana kuna wakati unafika unawaza ni njia gani utumie ili ufikie malengo yako. Kila mtu anawaza kufanikiwa kuwa na maisha mazuri kujenga familia bora kutunza wazazi wake vizuri n.k. Mafanikio ya malengo yako hayawezi kupatikana kwa kufanya jambo moja, lazima ufanye mambo mengi mazuri ili mwisho ufike mahali ambapo ulitarajia kufika. Hapa nimekuwekea baadhi ya mambo muhimu yanayoweza kuwa na mchango mkubwa katika safari yako kkuelekea kwenye mafanikio. Upekee. Katika dunia ya sasa yenye maendeleo na mapinduzi katika kila sekta, hakuna kazi au talanta(kipaji) ambacho kina watu wachache kila kazi au talanta ina watu wengi na ushindani mkubwa. Jambo la pekee linaloweza kukusaidia kwa sasa ni upekee, fanya kazi au talanta yako lakini kwa ubora na upekee na ubunifu wa hali ya juu kiasi kwamba utawavutia watu na kushinda ushindani uliopo. Albert Einstein aliwahi kusema “The woman who follows the crowd will usually go no further than the crowd. The woman who wa...

50 REASONS TO READ BOOKS FROM SPEAKING TREE BLOG

Join more than a thousand readers 1. Books help to feel more confident. 2. Books help to travel around the world in the cheapest way. 3. Books develop your personality. 4. Books provide food for thought. 5. Books make you laugh and think. 6. Books draw you towards perfection. 7. Books stimulate creativity. 8. Books bring out writing talent. 9. Books help in communicating. 10. Books clear your vision. 11. Books satisfy your curiosity. 12. Books help you make more choices. 13. Books help you build literary talent. 14. Books do not require any special device to teach. 15. Books increase your attention span. 16. Books are fruitful pastime. 17. Books can be used anytime, anywhere. 18. Books provide entertainment, when others fail. 19. Books make you powerful. 20. Books help you know the 'Whys' and 'Hows' of everything. 21. Books help you to create and spread fun. 22. Books help you travel across time intelligently. 23. Books keep you updated with f...

KUGHAIRISHA KWENYE FAIDA

Kughairisha mambo ndio tabia ambayo inaongoza kusababisha watu wengi kutofikia malengo yao kuliko tabia nyingine yeyote, pia tabia ambayo ni ngumu sana kuiacha kama umekwisha kuwa nayo. Kughairisha mambo hutokana na sababu mbalimbali, sababu kuu ikiwa ni kukosa motisha au msukumo wa ndani yako kufanya jambo, pia sababu nyingine kubwa ni kutopangilia mambo yako binafsi. Watu wengi sana huamini kughairisha ni kitu kibaya kabisa katika maisha, jambo ambalo sio kweli. Uzuri au ubaya wa kughairisha hutegemea jambo unaloghairisha, wakati unaoghairisha, na sababu ya kughairisha. Mara nyingi kughairisha hugharimu pale unapoghairisha kwa kutojisikia kufanya jambo bila sababu yoyote (uvivu wa kufanya). Je, unawezaje kupata faida kwa kughairisha? Mwandishi Brian Tracy katika kitabu chake cha Eat that Frog anasema, Kila mtu hughairisha lakini kinachotofautisha kati ya watu wanaofanikiwa na wasiofanikiwa ni katika mambo wanyoghairisha, wengi wasiofanikiwa hughairisha mambo ambayo huc...

SILAHA YA KUTOLAUMU KUFIKIA MAFANIKIO.

Kila jambo unalolifanya duniani linakuwa na asilimia kadhaa ya kushindwa, ndio maana watu huwa na plani B. Unaweza kufanya jambo kwa uhakika kabisa lakini kitu kidogo sana kikakufanya ushindwe, na hii ndio inafanya watu wafanye vitu kwa umakini na kufikiria sana hasa pale ambapo unania ya kufanikiwa katika mambo yako. Lakini muda mwingine unaweza kuwa umefanya jambo kwa umakini sana bila kukosea lakini ukashindwa kwasababu za mtu mwingine ambae mlikuwa mnashirikiana nae huenda ni kwa uzembe au bahati mbaya lakini mambo ndio yameharibika.  Lawama Katika hali kama hii ndipo watu huanza kutupiana lawama, huyu anamwambia mwingine “Unaona uzembe wako umetutia hasara”, Yule pia anatafuta sababu ya yeye kukosea, anaweza akatupia mpira kwa mwingine au la akalaumu vifaa alivyotumia au miundombinu, ilimradi asionekane mkosaji. Katika kampuni au madaraka Fulani watu hupenda kuwatupia lawama watu wa chini yao kimadaraka, lawama hizi huenda ngazi kwa ngazi mpaka kumfikia mtu wa ...

JOIN US ON TELEGRAM

JOIN US ON TELEGRAM
Join a thousand readers on telegram channel, start a reading habit, get inspired, motivated and learn to win in life.Click on the Image join us