Skip to main content

YAFAHAMU HAYA KUHUSU KUSAMEHE

Kusamehe ni kitendo cha kuondoa hasira, maumivu na hisia unazokuwa nazo baada ya kukosewa. Kila binadamu anapokosewa huona ameonewa na sio haki kile alichofanyiwa hivyo huwa na hasira na hisia za maumivu. Kila lile jambo au tendo linapojirudia akilini mwake hupata maumivu moyoni, hukosa furaha amani na hata kupata msongo wa mawazo.
Njia ya kuondokana na maumivu hasira na mawazo yote ni kusamehe. Hapa ndipo wengi huona ni jambo gumu, pale ambapo mtu amekukosea sana halafu wewe uje umsamehe kirahisi tu. Wengi huona sio haki na kuchukua uamuzi wa kulipiza kisasi. Yafahamu haya kuhusu kusamehe:-
 
1.      KUSAMEHE NI KUJIPENDA MWENYEWE
Unapotoa msamaha unaondoa hasira maumivu na mawazo yote uliyonayo juu ya Yule mtu alie kukosea, hivyo kuweka huru moyo wako na akili yako.  Kubaki na hasira, maumivu na hasira ni hasara kwako kwani huhatarisha afya yako.
2.      USISUBIRI MPAKA UOMBWE MSAMAHA
Watu wengi kusamehe mpaka waombwe msamaha, hilo halifai fikiria Yule aliekukosea asipokuomba msamaha  utaendelea kuteseka na mawazo mabaya na kutawaliwa na hasira mpaka lini?. Jambo la muhimu ni kusamehe hata kama hujaombwa msamaha maana ni faida kwako mwenyewe.
 
3.      KUSAMEHE SIO UJINGA
Mtu anaposamehe wengi hufikiria ni ujinga hasa vijana wa leo, pale mtu anapokukosea kosa kubwa halafu wanaona umemsamehe wao huona ni ujinga. Utwasikia wakisema “Ningekuwa mimi nisingemsamehe, ujinga huo” lakini ni kwasababu hawajui faida za kusamehe. Anaesamehe ana faida nyingi kuliko anaesamehewa.
4.      KUSAMEHE SIO UNYONGE
Pale inapotokea mkubwa wako amekukosea na ukamsamehe hata kabla hajakuomba msamaha, watu wengi hufikiria kuwa umemsamehe kwakuw wewe ni mnyonge kwake, jambo ambalo si sahihi. Kusamehe ni jambo la kishujaa na  ndio maana ni watu wachache wenye uwezo wa kusamehe, wengi katika nyakati za sasa hulipiza kisasii kwa kuwa ni wadhaifu mioyoni mwao (jambo wana nguvu za miili), hivyo hushindwa kusamehe.
5.      SIO LAZIMA KURUDISHA UHUSIANO WENU WA ZAMANI
Kama rafiki yako wa karibu amekusaliti kiasi cha kukuumiza moyo wako, ukimsamehe mnaweza mkarudisha urafiki wenu au msiurudishe. Pale ambapo unaona rafiki yako hatambui makosa aliyoyafanya na hana wasiwasi wala woga juu ya hilo, unaweza ukamsamehe halafu kila mtu akaishi maisha yake kwa amani.
6.      NI NJIA YA KUTAFUTA AMANI YA MOYO WAKO
Moyo wako ukiwa na msongo wa mawazo ni mateso sana kwako, hivyo samehe ili upate amani ya moyo na kuwa na utulivu akilini mwako hivyo kuendelea na kazi na mmipango yako kwa  amani na furaha.
7.      KUSAMEHE SIO JAMBO RAHISI
Kumsamehe mtu aliekukosea kunahitaji kujitoa moyoni kwani tukio huendelea kujirudia akilini mwako hivyo kurejesha kumbumbu za hasira na maumivu. Kusamehe kunahitaji utulivu wa kufikiria jambo na busara kukusaidia kutoa msamaha wa kweli.
Kusamehe ni ushujaa na ni watu wachache wenye uwezo wa kusamehe.
 

Dunia ingekuwa ni sehemu nzuri ya furaha kama kila mmoja angekuwa anasamehe, kwani matukio mengi mabaya kwa sasa ni kulipiza kisasi. Jiepushe na kutenda makosa na mtu akikukosea toa msamaha. Hiyo ni njia ya kuweka mahusiano mazuri ya kiimani katika dini

ANZA KUWA NA MAZOEA YA KUSAMEHE, MWISHO ITAKUWA NI UTARATIBU WAKO.

Comments

Popular posts from this blog

HATUA 10 ZA KUONGEZA UJASIRI BINAFSI

 Ujasiri ni imani anayokuwa nayo mtu juu ya kufanikiwa kwa lengo lake. Ujasiri huo unaweza ukawa ni wa kutegemea mtu au ujasiri binafsi  ambao unategemea  uwezo wa mhusika katika kutenda jambo flani. Ujasiri huleta furaha katika maisha na  pia huongeza ufanisi wa kazi unazofanya na pia mahusiano mazuri katika familia na jamii kwa ujumla.Ktokuwa na ujasiri hupunguza ufanisi wa kazi na huweza kusababisha msongo wa mawazo. 1.        JITAAMBUE Jichunguze na uweze kufahamu mambo ambayo wewe ni dhaifu na mambo yale ambayo wewe  ni hodari unaweza ukayafanya bila wasiwasi. Pia tambua  vitu gani unavipenda na vitu gani unavyovichukia, pia jitambue  wewe katika jamii unatazamwaje na watu na malengo yako kwa ujumla. Hayo yatakusaidia katika kuepuka mambo yatakayokupa huzuni hivyo kukudhoofisha. 2.        ANZA SIKU YAKO VIZURI Anza siku yako kwa kufuata ratiba ambayo umeipangilia na fuata...

MAMBO MUHIMU KWAKO KIJANA WA LEO.

Habari, najua kama wewe ni kijana kuna wakati unafika unawaza ni njia gani utumie ili ufikie malengo yako. Kila mtu anawaza kufanikiwa kuwa na maisha mazuri kujenga familia bora kutunza wazazi wake vizuri n.k. Mafanikio ya malengo yako hayawezi kupatikana kwa kufanya jambo moja, lazima ufanye mambo mengi mazuri ili mwisho ufike mahali ambapo ulitarajia kufika. Hapa nimekuwekea baadhi ya mambo muhimu yanayoweza kuwa na mchango mkubwa katika safari yako kkuelekea kwenye mafanikio. Upekee. Katika dunia ya sasa yenye maendeleo na mapinduzi katika kila sekta, hakuna kazi au talanta(kipaji) ambacho kina watu wachache kila kazi au talanta ina watu wengi na ushindani mkubwa. Jambo la pekee linaloweza kukusaidia kwa sasa ni upekee, fanya kazi au talanta yako lakini kwa ubora na upekee na ubunifu wa hali ya juu kiasi kwamba utawavutia watu na kushinda ushindani uliopo. Albert Einstein aliwahi kusema “The woman who follows the crowd will usually go no further than the crowd. The woman who wa...

50 REASONS TO READ BOOKS FROM SPEAKING TREE BLOG

Join more than a thousand readers 1. Books help to feel more confident. 2. Books help to travel around the world in the cheapest way. 3. Books develop your personality. 4. Books provide food for thought. 5. Books make you laugh and think. 6. Books draw you towards perfection. 7. Books stimulate creativity. 8. Books bring out writing talent. 9. Books help in communicating. 10. Books clear your vision. 11. Books satisfy your curiosity. 12. Books help you make more choices. 13. Books help you build literary talent. 14. Books do not require any special device to teach. 15. Books increase your attention span. 16. Books are fruitful pastime. 17. Books can be used anytime, anywhere. 18. Books provide entertainment, when others fail. 19. Books make you powerful. 20. Books help you know the 'Whys' and 'Hows' of everything. 21. Books help you to create and spread fun. 22. Books help you travel across time intelligently. 23. Books keep you updated with f...

KUGHAIRISHA KWENYE FAIDA

Kughairisha mambo ndio tabia ambayo inaongoza kusababisha watu wengi kutofikia malengo yao kuliko tabia nyingine yeyote, pia tabia ambayo ni ngumu sana kuiacha kama umekwisha kuwa nayo. Kughairisha mambo hutokana na sababu mbalimbali, sababu kuu ikiwa ni kukosa motisha au msukumo wa ndani yako kufanya jambo, pia sababu nyingine kubwa ni kutopangilia mambo yako binafsi. Watu wengi sana huamini kughairisha ni kitu kibaya kabisa katika maisha, jambo ambalo sio kweli. Uzuri au ubaya wa kughairisha hutegemea jambo unaloghairisha, wakati unaoghairisha, na sababu ya kughairisha. Mara nyingi kughairisha hugharimu pale unapoghairisha kwa kutojisikia kufanya jambo bila sababu yoyote (uvivu wa kufanya). Je, unawezaje kupata faida kwa kughairisha? Mwandishi Brian Tracy katika kitabu chake cha Eat that Frog anasema, Kila mtu hughairisha lakini kinachotofautisha kati ya watu wanaofanikiwa na wasiofanikiwa ni katika mambo wanyoghairisha, wengi wasiofanikiwa hughairisha mambo ambayo huc...

SILAHA YA KUTOLAUMU KUFIKIA MAFANIKIO.

Kila jambo unalolifanya duniani linakuwa na asilimia kadhaa ya kushindwa, ndio maana watu huwa na plani B. Unaweza kufanya jambo kwa uhakika kabisa lakini kitu kidogo sana kikakufanya ushindwe, na hii ndio inafanya watu wafanye vitu kwa umakini na kufikiria sana hasa pale ambapo unania ya kufanikiwa katika mambo yako. Lakini muda mwingine unaweza kuwa umefanya jambo kwa umakini sana bila kukosea lakini ukashindwa kwasababu za mtu mwingine ambae mlikuwa mnashirikiana nae huenda ni kwa uzembe au bahati mbaya lakini mambo ndio yameharibika.  Lawama Katika hali kama hii ndipo watu huanza kutupiana lawama, huyu anamwambia mwingine “Unaona uzembe wako umetutia hasara”, Yule pia anatafuta sababu ya yeye kukosea, anaweza akatupia mpira kwa mwingine au la akalaumu vifaa alivyotumia au miundombinu, ilimradi asionekane mkosaji. Katika kampuni au madaraka Fulani watu hupenda kuwatupia lawama watu wa chini yao kimadaraka, lawama hizi huenda ngazi kwa ngazi mpaka kumfikia mtu wa ...

JOIN US ON TELEGRAM

JOIN US ON TELEGRAM
Join a thousand readers on telegram channel, start a reading habit, get inspired, motivated and learn to win in life.Click on the Image join us